Hatua 5 muhimu zakuzingatia kabla yakununua nyumba

Kuongezeka kwa bei za nyumba katika miji mikubwa nchini hapa Australia, kunasababisha iwe vigumu kwa wanunuzi wa mwanzo kuingia katika soko hilo. Kujua kupanga bajeti na kufanya utafiti, inaweza saidia kupunguza usumbufu. Huu hapa ushauri huo:

Person holding small house in cupped hands

Person holding small house in cupped hands Source: AAP

1. Weka hela za akiba

Malipo ya asilimia 10 ya bei ya nyumba yanahitajika unapo nunua nyumba. Hata hivyo, wanunuaji wanaweza epuka malipo ya ziada kwa kampuni za dhamana zinazo kopesha hela zaku nunua nyumba iwapo wana weka asilimia 20 ya bei ya nyumba. Kama ume weka hela zakutosha, hatua inayo fuata ni ombi lako la mkopo kukubaliwa.

Image

2. Chunguza aina ya mikopo ya nyumba na hakikisha ombi lako la mkopo linakubaliwa.

Jua idadi ya hela unazohitaji kununua nyumba, kabla yaku amua aina ya mkopo unao hitaji, uliza watakao kupa mkopo huo wakupe maelezo kamili uyalinganishe na mikopo mingine ambayo iko sokoni.

Image

3. Kopa kulingana na mapato/uwezo wako.

Kuwa makini usikope zaidi ya uwezo wako. Haitakuwa vizuri kujipata katika hali ambayo unalazimishwa kuuza nyumba yako kwa sababu hauwezi timiza masharti yaku lipa mkopo wa nyumba.

Suburbs
Source: Getty Images

4. Wekeza hela kwa ripoti ya ukaguzi

Ukaguzi wa jengo huenda uka kugharimu ma mia ya dola ila, inaweza kuokolea maelfu ya dola kwaku epuka matatizo ukisha hamia ndani ya nyumba.

Dream Home
Source: Getty Images

5. Fanya bajeti kwa gharama za ziada

Hakikisha unafanya bajeti kwa gharama za ziada zinazo husiana na ununuaji wa nyumba kama ada za halmashauri, kodi za nyumba na kadhalika.

Image


Share

Published

By Ildiko Dauda
Presented by Frank Mtao

Share this with family and friends