Mwongozo wa Makazi: 10 muhimu kuhusu kiharusi

Kiharusi si mshtuko wa roho. Kiharusi hutokea wakati upatikanaji wa damu kwa ubongo unakatizwa ghafla. Ni muhimu kupata msaada wa haraka wa matibabu, kupona kiharusi.

Kiharusi

Source: Getty Images

1. Mmoja kati yawa Australia wasita, ata athiriwa na kiharusi katika maisha yake.

Stroke survivor

2. Mtu mmoja kati yawatu watatu hufariki ndani ya kipindi cha mwaka mmoja baada yaku athiriwa na kiharusi.

Stroke victim
Source: EPA

3. Kiharusi huwaua wanawake wengi kuliko saratani ya matiti na wanaume wengi zaidi kuliko saratani ya kibofu.

Men and women
Source: Getty Images

4. Asilimia 20 yawatu ambao huathiriwa na kiharusi huwa chini ya umri wa miaka 55.

Doctors
Source: Getty Images

5. Kuna uwezekano wanaume wanaweza athiriwa na kiharusi wakiwa na umri mdogo.

Young stroke victim
Source: AAP

6. Shinikizo ya damu ni moja ya athari kubwa zinazo julikana kusababisha kiharusi.

Shinikizo ya damu ni wakati shinikizo ya damu mwilini inazidi 140/90. Hali hii inajulikana kama hypertension au shinikizo ya damu. Kawaida shinikizo ya damu huwa 120/80.

Blood pressure
Source: Press Association

7. Mtihani unaojulikana kwa jina: FAST ni mbinu rahisi yakutambua naku kumbuka ishara za kiharusi.

Mtihani wa FAST unajumuisha maswali rahisi kama: Sura- tazama sura ya mwathiriwa. Mdomo wake ume pengama? Mkono- mwathiriwa anaweza inua mikono yote mbili? Matamshi- je matamshi yake ya maneno yame badilika nakuwa pole pole zaidi? Wanakuelewa? Wakati- Wakati ni muhimu. Ukiona dalili hizi, pigia simu 000 mara moja.

FAST
Source: Courtesy of Stroke Foundation

8. Ishara za kiharusi zinaweza tokea moja baada ya nyingine au kwa mchanganyiko.

Stroke brain scans
Source: Monty Rakusen/Getty Images

9. Baadhi ya tiba za kiharusi lazima zitolewe katika muda wa masaa 4.5 ya shambulizi la kiharusi kuanza, au wakati dalili za kiharusi zina jitokeza.

Ambulance emergency
Source: AAP

10. Ni muhimu kupokea matibabu ya dharura

Kama unakabiliwa na kiharusi, matibabu ya dharura yanaweza okoa maisha yako na yanaweza punguza uwezekano wa uharibifu wakudumu wa ubongo. Daktari ndiye anaweza amua kama unakabiliwa na kiharusi ama ulikabiliwa na kiharusi.

Emergency
Source: AAP

Kama unahitaji huduma ya mkalimani, pigia simu huduma yawakalimani kwa namba hii: 13 14 50, sema lugha unayo hitaji, subiri hadi mkalimani atakapo jumuishwa katika simu.

 


Share

Published



Share this with family and friends