Mwongozo wa makazi: Mambo 10 muhimu ya wazazi kuzingatia kabla yaku jadili mihadarati na wanao

Kuzungumzia utumiaji wa mihadarati huwa changamoto kwa sababu ya unyanyapaa unao husishwa na mihadarati miongoni mwa jumuiya kadhaa. Hizi hapa mbinu 10 zaku wahamasisha watoto wako wajadili kuhusu mihadarati nawe.

Mihadarati

Mihadarati Source: Getty Images

1. Husika katika maisha yao

Fuatilia maslahi yao na panga ratiba yaku jumuika nao kila mara. Nimu himu kufanya vitu pamoja kama familia, kwa mfano kula pamoja kila siku.

Be an active part of their lives
Source: Getty Images

2. Sikiliza watoto wako

Wahamasishe wachangie matatizo yao nawe, bila kuwa na wasiwasi. Omba mchango wao katika uamuzi wa maswala ya familia, ili wahisi unathamini maoni yao.

Listen to your kids
Source: Getty Images

3. Kuwa mfano mzuri

Ni muhimu kuto puuza ushawishi wa tabia yako kwa watoto wako, haswa kwa maswala ya pombe, tumbaku au kutumia madawa vibaya.

Be a role model
Source: Getty Images

4. Kuwa mwaminifu nao

Hauta jua kila kitu kinacho husiana na mihadarati. Ukiwa mwaminifu na wazi kuhusu msimamo wako, itakuwa rahisi kwa watoto wako kuwa waaminifu nawe.

Be honest with your kids
Source: Getty Images

5. Chagua wakati vizuri

Hakikisha unachagua wakati mzuri waku jadili mihadarati na watoto wako. Huenda ikawa wakati mna tazama runinga, au wanapo zungumza kuhusu mtu mwingine katika shule yao au katika kundi lao la marafiki.

Pick your moment
Source: AAP

6. Kuwa mtulivu

Ni muhimu kuwa na mantiki na utulivu katika mjadala kuhusu mihadarati, pamoja nakuto kasirika haraka. Usiwakejeli wanao, kwa sababu hali hiyo inaweza fanya mijadala ya usoni kuhusu mihadarati kuwa migumu.Image

7. Epuka migogoro

Nivigumu kutatua tatizo wakati kuna mgogoro. Iwapo mgogoro unazuka, sitisha mazungumzo, hadi nyote mtakapo tulia.

Avoid conflict
Source: Pixabay/Public Domain

8. Endeleza mazungumzo

Unapo fanya mazungumzo ya kwanza kuhusu mihadarati, ni muhimu kuendeleza mjadala huo. Anza kuzungumza na watoto wako kuhusu mihadarati mapema, pia kuwa tayari kuzungumza na watoto wako kuhusu swala hili wakati wowote.

Keep talking
Source: Getty Images

9. Weka mipaka iliyo wazi

Jadili na kubaliana na watoto wako jinsi watafanya, watakapo jipata katika mazingira ambako kuna mihadarati. Kwa mfano, hakikisha wanajua utaenda kuwachukua iwapo wanahitaji msaada wakati wowote. Hata hivyo, hakikisha wanaelewa kuwa, ungependelea wasijiweke katika mazingira ambako huenda waka kabiliana na mihadarati.

Set clear boundaries
Source: Getty Images

10. Lenga mambo chanya.

Wahamasishe wajihisi vizuri, na hakikisha wanajua kuwa wanastahili kuheshimiwa, na pia wana stahili kujiheshimu.

Image

Katika kila mkoa na jimbo kuna vituo vya maelezo kuhusu pombe na mihadarati.Vituo hivyo hutoa ushauri, rufaa na tathmini masaa 24 kila siku. Wanatoa huduma kwa watu binafsi, familia, marafiki, wataalam wa jumla, wataalam wengine wa afya, biashara na makundi mengine ya jumuiya.


Share

Published

Updated

By Ildiko Dauda


Share this with family and friends