Tanzania yakaribishwa katika kombe la Afrika kwa kichapo

Tanzania ndiye nchi pekee kutoka Afrika Mashariki inayo shiriki katika michuano ya Kombe la Afrika nchini Ivory Coast.

Wachezaji 11 wa Taifa Stars walio anza mechi dhidi ya Morocco katika kombe la Afrika nchini Ivory Coast
Tanzania ili orodheshwa katika Kundi F pamoja na Morocco, Zambia na DR Congo.
Morocco yaifanyia Tanzania unyama katika kombe la Afrika
Katika mechi ya kwanza ya kundi hilo Morocco ilionesha ubabe wake kwa kuicharaza Taifa Stars magoli 3 bila jibu.
Charles M'Mombwa (katikati) katika mechi dhidi ya Morocco.jpg
Licha ya kichapo hicho, mamia yama shabiki wa Taifa Stars wanao ishi Australia, wali amkia mechi hiyo mapema kumshabikia Charles Kokola M'Mombwa aliye dhihirisha kuwa anastahili kiwango chakucheza dhidi ya wachezaji wa Morocco wenye majina tajika katika soka yakimataifa.

Kupitia matokeo hayo hasi, sasa Tanzania lazima ioneshe viwango vya juu zaidi iwapo ina matumaini yaku fuzu kutoka kundi hilo.

Share

Published

Updated

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS

Share this with family and friends