Maandamano ya upizani DRC yatishia kuapishwa kwa Rais Tshisekedi

Felix Tshisekedi Tshilombo atangazwa rais mteuli wa DR Congo

Felix Tshisekedi Tshilombo atangazwa rais mteuli wa DR Congo Source: AP

Wawili kati ya wagombea wakuu wa upinzani kwenye uchaguzi wa Disemba mwaka jana nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wameitisha maandamano Jumamosi wakati wa kuapishwa kwa Rais Felix Tshisekedi kuongoza muhala wa pili.


Tshisekedi alishinda kwa kishindo uchaguzi wa tarehe 20 Disemba, lakini uchaguzi huo uligubikwa na madai mengi ya udanganyifu, changamoto za kiufundi na kasoro nyingine.

Viongozi wawili wa upinzani, Martin Fayulu na Moise Katumbi pamoja na wapinzani wengine, waliomba uchaguzi mpya, ombi ambalo lilitupiliwa mbali na serikali.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share