Jimbo la Queensland limejiunga na majimbo mengine kutia saini mkataba na serikali ya shirikisho, kuwekeza kikamilifu shule za umma kufikia mwaka wa 2034.
Watu sita wameuawa katika shambulizi linalodaiwa kufanywa na wanamgambo wa al-Shabaab kwenye kituo cha polisi kaskazini-mashariki mwa Kenya, Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mamlaka nchini Kenya.
Wakuu wa nchi toka jumuiya ya Afrika Mashariki na ile ya maendeleo ya kusini mwa Afrika, SADC, watakutana hivi leo kwa njia ya mtandao, kujadiliana kuhusu hali inayoendelea mashariki mwa nchi ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.