Canberra: Tathmini ya wiki 20 Julai 2018

Peter Dutton amependekeza kupunguza kiwango cha mapokezi ya wahamiaji nchini Australia

Waziri Mkuu wa Australia Malcolm Turnbull na waziri wa maswala ya nyumbani Peter Dutton wazungumza na waandishi wa habari mbele ya bunge la taifa mjini Canberra Source: AAP Image/Lukas Coch

Wakati wanasiasa wanaendelea kupiga kampeni nchini kote kabla ya wikendi ya chaguzi ndogo tano, serikali haikuweza epuka baadhi ya maswala tata yaliyo tawala mwaka huu.


Mradi wa uhamiaji wa waziri mkuu wa Australia, pamoja na sera ya nishati mara nyingine zilikuwa kwenye ajenda ya kampeni.

Na katika taarifa zingine, mawaziri wa nishati wa mikoa na majimbo, watakutana mwezi ujao kushauriana kuhusu msimamo wao, kwa sera ya dhamana ya nishati ya taifa toka kwa serikali ya mseto.

Mawaziri hao hawatakuwa na uhaba wa vitu vyakusoma kabla ya mkutano huo kwa mfano; ripoti tatu muhimu zime tolewa kuhusu nishati, pamoja na uchunguzi ulio fanywa na serikali.

 

 

 


Share