Jamii ya Kitwek yawakaribisha wahitimu wamafunzo yakitamaduni

Vijana kutoka jamii ya Kitwek mjini Perth, wakaribishwa katika sherehe baada ya tohara na kukamilisha mafunzo.

Vijana kutoka jamii ya Kitwek mjini Perth, wakaribishwa katika sherehe baada ya tohara na kukamilisha mafunzo. Source: Kitwek Association

Jamii nyingi za watu wenye asili ya Afrika zina mila, desturi na tamaduni zao, ambazo kwa sehemu kubwa zinatofautiana.


Katika jimbo la Magharibi Australia, Jamii ya Kitwek alikabiliwa na changamoto yaku endeleza tamaduni zao hususan kwa swala la tohara ya wavulana.

Licha ya nia yakushiriki kuwepo kutoka kwa wahusika, uwezo wakusafiri hadi nchini Kenya haukuwepo kwa sababu yakufungwa kwa mipaka yakimataifa ya Australia kwa sababu ya UVIKO-19. Hali hiyo iliwalazimisha viongozi wa jamii ya Kitwek kutafuta mbinu mbadala yakuwatendea vijana wao haki.

Katika mazungumzo maalum na Idhaa ya Kiswahili ya SBS Rais wa jamii ya Kitwek Bw Steven Sitienei, alifunguka kuhusu jinsi kamati yake ya viongozi ilivyo tatua changamoto hiyo. Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share