Kauli ya mwanae Museveni yazua kero kwa majirani Sudan na DRC

Lt.Gen. Muhoozi Kainerugaba akitoa hotuba.jpg

Serikali ya Sudan inaitaka Uganda iombe rasmi msamaha, kutokana na kile imekitaja kuwa ujumbe wa kuchukiza na hatari ulioandikwa na mkuu wa jeshi la Uganda Jenerali Muhoozi Kainerugaba, aliyetishia kuivamia Khartoum kijeshi.


Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vile vile, imemuita balozi wa Uganda nchini humo, kutokana na ujumbe wa Kainerugaba ambapo ametishia pia kuvamia eneo la mashariki mwa DRC.

Kainerugaba, mtoto wa rais Yoweri Museveni, aliandika ujumbe kwenye mtandao wa X Jumanne, akitishia kuivamia na kuiteka Khartoum kwa msaada wa rais mteule wa Marekani Donald Trump, atakapoingia ofisini. Baadaye aliufuta ujumbe huo.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share