Shinikizo dhidi ya uongozi wa Malcolm Turnbull la ongezeka

Peter Dutton (kulia) na Malcolm Turnbull (kushoto) kabla ya Dutton kuwania wadhifa wa waziri mkuu

Peter Dutton (kulia) na Malcolm Turnbull (kushoto) kabla ya Dutton kuwania wadhifa wa waziri mkuu dhidi ya Waziri Mkuu Malcolm Turnbull Source: AAP

Waziri Mkuu Malcolm Turnbull, amekana kazi yake iko mashakani, baada yakupona kura dhidi ya uongozi wake, toka kwa aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Peter Dutton.


Kwa sasa Bw Turnbull lazima afanyie mageuzi, baraza lake la mawaziri baada ya mawaziri kadhaa kuwasilisha barua zaku jiuzulu kufuatia matokeo ya kura ya uongozi kutangazwa.

Mwandishi wa SBS Swahili Frank Mtao alizungumza na Bw Peter Gitonga, ambaye ni mwanasheria maarufu na mtaalam wa maswala ya uongozi. Bw Gitonga alichambua masaibu yanayo mkumba Bw Turnbull ndani ya chama chake cha Liberal.


Share