Waziri Mkuu Anthony Albanese na kiongozi wa upinzani Peter Dutton wana fanya kampeni katika siku ya mwisho ya kampeni za uchaguzi mkuu kabla ya vituo vya kupiga kura kufunguliwa rasmi kesho.
Polisi nchini Kenya imesema mauaji ya mbunge wa Kenya, Charles Ong'ondo Were, katika mji mkuu Nairobi, yumkini yalikuwa ni ya kupangwa. Mbunge huyo, alipigwa risasi na kuuawa barabarani kwenye mji mkuu wa Nairobi jana Jumatano. Akilielezea tukio hilo msemaji wa Polisi ya Kenya Muchiri Nyaga amesema kwa namna tukio hilo lilivyotokea inaonekana kwamba uhalifu huo ulipangwa.
Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.