Jamii zawa hamiaji za dai kuwa, viza mpya ya wazazi ya Australia haiko sawa

Familia ya Sandhu katika picha

Familia ya Sandhu katika picha Source: Sandhu

Get the SBS Audio app

Other ways to listen


Published

By Lin Evlin
Presented by Gode Migerano
Source: SBS


Share this with family and friends


Jumatano tarehe 17 Aprili, huduma ilifunguliwa kupokea maombi, ya viza ya muda mfupi ya wazazi, iliyo subiriwa kwa muda mrefu. Lengo la viza hiyo nikutoa uamuzi mbadala ya viza zakudumu zilizopo kwa wazazi wa wahamiaji.


Jamii zawa hamiaji zimefanyia kampeni kwa miaka mingi swala la viza zamuda mrefu, ambazo zinaweza ruhusu familia kuungana nama bibi nama babu wao ila, wahamiaji wengi wanasema wana hisi wanatengwa kupitia masharti magumu ambayo yame wekwa katika viza hiyo mpya.

Licha ya malalamishi hayo, serikali imesema kuwa viza hiyo ili undwa kupitia ushauriano na jamii, na kigezo cha mapato kipo, kuhakikisha mdhamini ana rasilimali zakutosha, kuwasaidia wazazi wake. David Coleman ndiye waziri wa uhamiaji wa shirikisho, ame eleza shirika la habari la SBS kuwa: Viza hiyo mpya itawasaida maelfu ya familia zawa Australia na, imefanikiwa kuwasilishwa na serikali licha ya upinzani unao endelea kutoka chama cha Labor.

Chama cha Labor kime kosoa sera hiyo ya chama cha mseto na, chama hicho kinatarajiwa kutangaza sera yake binafsi katika kampeni ya uchaguzi mkuu.


Share