Taarifa ya Habari 4 Septemba 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Get the SBS Audio app

Other ways to listen


Published

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS

Share this with family and friends


Mpango wa chama cha Labor kuzuia waajiri, kufuta makubaliano ya ajira yakasirisha upinzani wa shirikisho.


Upinzani wa shirikisho unaishtumu serikali kwakujaribu kushawishi mwamuzi huru wa ajira, baada yaserikali kutoa onyo kwa mipango yakujaribu kupunguza mamlaka ya waajiri kufuta mikataba ya kazi. Hata hivyo, waziri Brendan O'Connor ametupilia mbali madai ya upinzani.

Mashauriano juu ya mamlaka ya mikataba na kanuni za mapambano zinachelewesha kupelekwa kwa wanajeshi huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo chini ya jeshi la dharura la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Gazeti la The East Africa linafahamu kuwa nchi tano kati ya sita wanachama wa EAC – ikiwemo Kenya, Tanzania, Uganda na Sudan Kusini – ziko tayari kupeleka majeshi huko mashariki mwa DRC lakini zimesisitiza kuwepo kwa kanuni sahihi ili kuepuka makosa yaliyotokea katika vikosi vya awali vya kulinda amani.

Wakenya ndani na nje ya nchi waendelea kusubiri kujua kama uchaguzi wa urais utarudiwa au ushindi wa Dr William Ruto utaidhinishwa. Baada ya wiki nzima ya kila upande kutoa maombi na mawasilisho mbele ya majaji saba wa mahakama ya upeo, ngoja ngoja ya siku 14 sasa itafika tamati kesho ,Jumatatu tarehe 5.


Share